TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Pande hasimu Mali zasaini makubaliano ya amani

Pande hasimu Mali zasaini makubaliano ya amani Serikali na makundi sita ya wabeba silaha nchini Mali, yametia saini makubaliano ya amani yenye lengo la kuhitimisha machafuko kaskazini mwa nchi hiyo. Makubaliano hayo yametiwa saini leo huko Algiers, mji mkuu wa Algeria. Inaelezwa kuwa Harakati ya Kitaifa ya Ukombozi wa Azawad imekataa kutia saini makubaliano hayo. Habari zinasema kwamba, kundi hilo limetaka muda zaidi kwa ajili ya kufanya mazungumzo na makundi mengine. Maeneo ya kaskazini mwa Mali yamekuwa yakishuhudia machafuko tangu kulipojiri mapinduzi ya kijeshi dhidi ya serikali kuu ya nchi hiyo hapo mwaka 2012. Mazungumzo ya amani ya Mali yalianza mwezi Julai mwaka jana chini ya upatanishi wa Algeria. Jana Jumamosi waungaji mkono wa harakati za upinzani dhidi ya serikali waliandamana katika kulalamikia mwenendo mzima wa mazungumzo hayo. Inaelezwa kuwa, makubaliano hayo yamefikiwa ikiwa ni baada ya duru tano za mazungumzo.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)