TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Magaidi 8 wa Al-Shabab wauawa vitani Bakool, Somalia

Magaidi 8 wa Al-Shabab wauawa vitani Bakool, Somalia Wapiganaji 8 wa kundi la kigaidi Al-Shabab wameuawa baada ya kushambuliwa na vikosi vya serikali vikisaidiwa na vya Umoja wa Afrika katika jimbo la Bakool kusini magharibi ya Somalia. Akizungumza na waandishi wa habari, kamanda wa jeshi la Somalia katika eneo hilo Abdirahman Mohammed amesema oparesheni hiyo ya pamoja iliyodumu kwa saa 10 ilifanyika Ijumaa katika mji wa Celbaar. Mohamed amesema wanajeshi watatu wameuawa na wengine 15 kujeruhiwa kwenye mapambano hayo. Hata hivyo kundi la Al-Shabab limedai kuwa zaidi ya wanajeshi 10 wa serikali wameuawa na kusisitiza kuwa bado wanaudhibiti mji huo. Wakati huo huo afisa wa serikali ya Somalia amesema vikosi vya serikali tayari vimerudi kwenye kambi yao baada ya shambulizi hilo. Vikosi vya Somalia vikisaidiwa na vya Umoja wa Afrika AMISOM vimepata mafanikio makubwa katika mwaka mmoja uliopita kwa kunyakua miji mikubwa kutoka kwa wapiganaji wa Al-Shabab
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)