TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Kuna wapiganaji 5, 000 wa kigeni nchini Libya

Kuna wapiganaji 5, 000 wa kigeni nchini LibyaWaziri wa mambo ya nje wa Libya Mohamed al-Dairi amesema kuna wapiganaji 5, 000 wa kigeni nchini humo na kutoa wito wa msaada wa kimataifa katika kupambana na ugaidi.
Waziri huyo amenukuliwa akisema kiongozi wa kundi la kigaidi la Emir ambalo lina uhusiano na lile la Daesh  (ISIL) nchini Libya lililohusika na mashambulizi ya mabomu mjini al-Gubba ni raia wa Yemen. Al-Dairi pia ametoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kutoa silaha kwa jeshi la Libya akisistiza kuwa tishio la kigaidi sio tu ni kwa Libya bali pia eneo lote la kaskazini mwa Afrika na bara Ulaya. Mipaka ya Libya isiokuwa na doria kali imewezesha wapiganaji kuingia nchini humo wakitokea Nigeria, Mali na Niger.
Huku hayo yakijiri kuna ripoti kuwa Italia inatuma vikosi vya kijeshi  nchini Libya kulinda maslahi yake nchini humo. Gazeti la nchini Italia la La Stampa  limesema askari wa kikosi maalumu cha Italia wanafanya mazoezi ya kukabiliana na magaidi wa Daesh nchini Libya. Imearifiwa kuwa Italia na wasi wasi mkubwa kuwa magaidi wa Daesh wanaweza kuvuriga bomba la gesi litokalo Libya na kupitia chini ya bahari hadi kusini mwa nchi hiyo ya Ulaya.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)