TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Pinda ahimiza elimu ya athari za madawa ya kulevya

Pinda ahimiza elimu ya athari za madawa ya kulevyaWaziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amewataka viongozi wa dini zote katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki, waitumie mikutano yao ya mahubiri kutoa elimu juu ya athari za madawa ya kulevya kwa waumini wao na Watanzania wote kwa ujumla.
Mizengo Pinda amesema kuwa, anawaomba viongozi wa dini nchini Tanzania kuungana na serikali kwa ajili ya kutoa elimu juu ya athari za biashara ya madawa ya kulevya na matumizi yake katika jamii. Ameongeza kuwa, kampeni hiyo inapaswa kuanzia misikitini, makanisani na kwenye mikutano yote inayofanywa na viongozi wa dini na wa serikali.
Aidha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesisitiza kuwa, viongozi wa dini wana jukumu kubwa la kuwalea zaidi vijana ili wasijiingize kwenye matumizi ya madawa ya kulevya kwa sababu wao ndiyo kundi kubwa zaidi miongoni mwa waumini.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)