TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

UNHCR: Wakimbizi wa Somalia waondoke Kenya kwa hiari

UNHCR: Wakimbizi wa Somalia waondoke Kenya kwa hiariKamishna mkuu wa Tume ya Umoja wa Mataifa ya kuhudumia wakimbizi UNHCR António Guterres amesisitiza kurejea kwa hiari kwa wakimbizi wa Somalia walioko kwenye kambi za Dadaab nchini Kenya. Guterres ameyasema hayo baada ya kuzuru Dadaab iliyo katika Kaunti ya Garissa kaskazini mwashariki mwa Kenya ambayo ni kambi kubwa zaidi duniani ya wakimbizi ikiwa na zaidi ya wakimbizi 350, 000 kutoka Somalia.
Amesema sehemu muhimu ya ziara yake nchini Kenya ni kuanzisha maelewano imara na serikali ya Kenya kuhusu hali ya baadaye ya wakimbizi wa Somalia walioko nchini humo. Guterres amesisitiza kuwa kurejea nyumbani kwa wakimbizi hao kunapaswa kuwa kwa hiari kulingana na makubaliano ya pande tatu ambazo ni Somalia, Kenya na UNHCR ili kuhakikisha usalama na hadhi ya wakimbizi hao.  Mkuu wa UNHCR amesema pia wamefanya mawasiliano sawa na hayo na rais wa Somalia na wakuu wa  eneo la Juba Land.  Katika mkutano wake na Guterres Mei sita mjini Nairobi, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya alisema, uharaka wa kuwarudisha wakimbizi umesababishwa na tishio la kiusalama linaloikabili Kenya, na kuongeza kuwa, anataka mchakato huo ufanyike vizuri bila ya kusababisha matatizo. Serikali ya Kenya ilitangaza mwezi uliopita uamuzi wa kurejesha nyumbani wakimbizi wa Somalia kufuatia mauaji ya kigaidi kwenye chuo cha Garrisa ambapo watu 148 waliuwawa na zaidi ya 70 kujeruhiwa.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)