TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Wasomali waandamana kulaani askari wa AMISOM

Wasomali waandamana kulaani askari wa AMISOM Wasomali wa kusini magharibi mwa nchi hiyo wamefanya maandamano wakilalamikia ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa na askari wa kulinda amani wa Umoja wa Afrika nchini humo (AMISOM).
Maandamano hayo yalifanyika jana katika mji wa Hudur, makao makuu ya eneo la Bakool huko kusini magharibi mwa Somalia. Naibu gavana wa mkoa wa Bakool, Abdullah Ahmad Noor amewaambia waandishi habari kwamba kuna tetesi kuwa askari wa Kiafrika wa kulinda amani nchini Somalia wamehusika na mauaji ya raia wa Somalia katika mji wa Hudur. Amesisitiza kuwa serikali ya Mogadishu imechukua uamuzi wa kuchunguza madai hayo.
Habari nyingine kutoka Somalia zinasema kuwa jeshi la serikali limewatia nguvuni watu 80 wanaodhaniwa kuwa wapiganaji wa kundi la kitakfiri la al Shabab. Wapiganaji wengine 24 wa kundi hilo wamejisalimisha wenyewe kwa polisi ya Somlai na kuliasi kundi hilo.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)