TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Algeria na Kenya kushirikiana katika uzalishaji mafuta

Algeria na Kenya kushirikiana katika uzalishaji mafuta Serikali ya Algeria na Kenya zimesaini makubaliano ya kushirikiana katika sekta ya usalishaji mafuta na gesi. Makubaliano hayo yalitiwa saini na Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Kenya, Amina Mohamed huku Algeria nayo ikiwakilishwa na Ramtane Lamamra, Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo. Kwa mujibu wa makubaliano hayo yaliyotiwa saini huko Algiers, mji mkuu wa Algeria, katika kuboresha na kuchochea ustawi wa viwanda na kiuchumi, nchi hizo zitashirikiana pamoja katika masuala ya uzalishaji wa mafuta na gesi pia. Makubaliano hayo kati na Nairobi na Algiers yanajumuisha pia usimamiaji na uwekaji sheria katika sekta ya mafuta, gesi na nishati, uvumbuzi na uzalishaji vyanzo vya hydrocarbon nchi kavu na baharini, kupanua viwanda vya petrokemikali, shughuli za ujenzi wa vinu, kutafuta soko la ndani, usafirishaji na usambazaji wa mafuta hayo. Hivi karibuni serikali ya Kenya ilitangaza kuwa inatazamiwa kuanza kuuza mafuta ghafi ya petroli katika soko la kimataifa mwaka ujao na hivyo kuitangualia nchi jirani ya Uganda ambayo iligundua mafuta miaka tisa iliyopita.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)