TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Senegal yakosoa udhalilishaji wa Wade kwa Rais Sall

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhD7fKBh-y1apLJL2RAoHM6_Ex-tKO07qbq5DFSRm6X46h1e06RRjp5hmRWbuYW3ZfOAajA7uBN0TKs8grRtuuylXH5FguQG_YxTGrM4z-pHZrONm_5S_sQ5fFYIl7CttjUWZqNL7-jhds/s1600/wade.jpgChama tawala nchini Senegal kimekosoa utovu wa nidhamu wa rais wa zamani wa nchi hiyo Abdoulaye Wade dhidi ya Rais Macky Sall. Viongozi wengi wa serikali mbali na kukosoa matamshi ya Wade dhidi ya Rais Sall, wamemtaja Wade kuwa ni mtu aliyechanganyikiwa kutokana na uzee. Waziri Mkuu wa zamani wa Senegal kutoka chama tawala, Aminata Touré amesema kuwa matamshi ya Abdoulaye Wade yanapingana na mafundisho ya dini ya Kiislamu. Naye kwa upande wake Youssou Ndour Waziri Mshauri wa serikali ya Rais Macky Sall amekosoa vikali mwenendo wa rais huyo wa zamani wa Senegal na kuyataja matamshi yake kuwa hatari. Hivi karibuni Abdoulaye Wade alimtusi Rais Sall kwamba wazazi wake walikuwa watumwa na wala nyama za watu, hatua ambayo ameichukua katika kulalamikia kitendo cha kuzuiliwa mwanawe katika korokoro za serikali kutokana na tuhuma za ufisadi wa mali za umma. Karim Wade mwana wa Abdoulaye Wade ametupwa korokoroni tangu mwaka 2013 kwa kosa hilo huku kesi yake ikiwa bado inaendelea. Shirika la haki za binaadamu nchini Senegal, limeonyeshwa kusikitishwa na matamshi ya raia huyo wa zamani na kusema kuwa, hakuna njia nyengine ya kuweza kutetea matamshi hayo.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)