TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

B/H yaua makumi Nigeria kwa kuwakata na shoka

B/H yaua makumi Nigeria kwa kuwakata na shoka Wanamgambo wa wa Boko Haram, wameshambulia vijiji kadhaa kaskazini mashariki mwa Nigeria. Duru za habari za kieneo zimearifu kuwa, katika mashambulizi hayo yaliyotokea kwenye vijiji hivyo vya karibu na mpaka wa Cameroon, wanamgambo hao wamefanya mauaji ya kutisha kwa kutumia mashoka na kuchoma moto makazi ya raia. Kundi hilo lenye mafungamano na kundi la kitakfiri la Daesh, limefanya mashambulizi hayo kama ulipizaji kisasi kufuatia mashambulizi ya jeshi la Chad dhidi ya ngome za Boko Haram, mashambulizi ambayo yalipelekea makumi ya wanamgambo wa kundi hilo kuuawa. Inaelezwa kuwa, zaidi ya vijiji 10 vya jimbo la Borno vinaendelea kudhibitiwa na kundi hilo huku makumi ya wakazi wake wakiuawa kwa kukatwa na shoka. Mamia ya wakazi wengine wa vijiji hivyo wamelazimika kuwa wakimbizi nchini Cameroon. Tayari jeshi la Chad limejibu hujuma hiyo kwa kushambulia maeneo ya wanachama wa kundi hilo huko kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)