TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Marekani kufungua ubalozi wake Cuba

Marekani inasema kuwa itafungua ubalozi wake nchini Cuba kuanzia mwezi Aprili.
Baada ya duru ya pili ya mazungumzo mjini Washington yenye lengo la kurejesha uhusiano kati yao mwanadiplomasia wa cheo cha juu wa Marekani katika nchi za Marekani ya kusini Roberta Jacobson, alisema kuwa itawezekana kufunguliwa kwa ubalozi kabla ya mkutano wa kimaeneo ambao utafanyika nchini Panama kuanzia tarehe kumi mwezi Aprili.
Mkuu wa ujumbe wa Cuba Josefina Vidal alisisitiza kuwa Marekani ni lazima iondoe Cuba kutoka kwa orodha ya nchi ambazo zinaunga mkono Ugaidi kabla ya kurejesha tena uhusiano huo.
Mwezi Disemba Cuba na Marekani walitangaza kuwa walikubaliana kuboresha uhusiano wao baada ya zaidi ya miaka 50 .
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)