TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Chama cha Juwa chashinda tena uchaguzi Comoro

https://c1.staticflickr.com/3/2308/2361611730_f602dfe0e0.jpgMatokeo ya awali yaliyotangazwa na tume ya uchaguzi nchini Komoro yanaonyesha kuwa chama cha Juwa chenye misimamo ya Kiislamu na kinachoongozwa na Rais wa zamani Ahmad Abdullah Sambi, kimeshinda katika maeneo mbalimbali ya nchi kikifuatiwa na chama cha ‘Maelewano ya Wakomoro’. Kwa mujibu wa tume hiyo ya uchaguzi, matokeo rasmi yatatangazwa mwezi Machi mwezi ujao. Ushiriki wa wananchi katika uchaguzi huo uliofanyika siku ya Jumapili, ulifikia asilimia 73. Aidha theluthi moja kati ya wabunge 24 waliochaguliwa katika uchaguzi huo, wanatoka chama cha Juwa. Chama cha Ahmad Abdullah Sambi, rais wa zamani wa Comoro, kilikuwa madarakani hadi mwaka 2011. Kwa upande mwingine, chama cha Maelewano kwa ajili ya Wakomoro kilichoshika nafasi ya pili, ni moja ya waitifaki wakubwa wa chama cha Juwa. Ushindi huo unatajwa kuwa pigo kwa chama tawala cha UPCD ambapo hakuna mgombea hata mmoja kwa tiketi ya chama hicho aliyeshinda uchaguzi huo. Uchaguzi huo ulisimamiwa na waangalizi kutoka nchi zenye kuzungumza lugha ya Kifaransa na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)