TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

DRC yakosolewa kuwafunga watetezi wa haki

Mashirika kadhaa ya kutetea haki za binaadamu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zimeikosoa  
DRC yakosolewa kuwafunga watetezi wa haki   serikali ya nchi hiyo kwa kuwafunga wanaharakati wa haki za binaadamu. Zaidi ya taasisi 30 za kutetea haki za binaadamu nchini humo mapema leo zimeikosoa serikali hiyo kwa kuendelea kumshikilia korokoroni Christopher Ngoy Mutamba, mwanaharakati wa haki za binaadamu aliyetiwa mbaroni tarehe 21 mwezi Januari mwaka huu. Aidha mashirika hayo yameonyesha wasi wasi wao kuhusiana na kukosekana uadilifu katika uendeshaji wa kesi ya mtuhumiwa huyo. Wasiwasi huo umekuja kufuatia mahakama moja ya nchi hiyo kutangaza kuendelea kumshikilia Mutamba kwa muda zaidi. Mutamba alitiwa mbaroni tarehe 21 katika machafuko yaliyopelekea watu 42 kuuawa na mamia ya wengine kutiwa mbaroni na polisi ya nchi hiyo. maandamano hayo yaliibuka kupinga mpango wa mabadilisho ya kuendelea kusalia madarakani Rais Joseph Kabila wa nchi hiyo.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)