TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

LEO KATIKA HISTORIA Jumatano, Februari 18,

Jumatano, Februari 18, 2015
Leo ni Jumatano tarehe 28 Rabiuthani 1436 sawa na 18 Februari 2015.
Siku kama ya leo miaka 50 iliyopita nchi ya Gambia ilifanikiwa kupata uhuru kutoka kwa mkoloni Mwingereza. Gambia ilikuwa koloni la kwanza la Uingereza barani Afrika. Uingereza iliikoloni nchi hiyo mwaka 1588 na kuendelea kupora maliasili za nchi hiyo kwa karibu karne nne. Mwaka 1963 Uingereza ambayo ilidhoofika kisiasa na kiuchumi kutokana na athari za Vita vya Pili vya Dunia haikuwa tena na uwezo wa kuendelelea kuikoloni Gambia na nchi hiyo ikapata utawala wa ndani. Mwaka 1965 katika siku kama ya leo Gambia ilijipatia uhuru wake.
Siku kama ya leo miaka 181 iliyopita sawa na tarehe 18 Februari mwaka 1834 vikosi vya majeshi ya Ufaransa ambavyo vilianza kuikalia kwa mabavu Algeria mwaka 1830, vilishindwa vibaya na wapiganaji wa Amir Abdulqadir Al Jazairi. Kushindwa huko kulipelekea theluthi moja ya askari wa Ufaransa kuuawa na nusu ya waliobakia kukamatwa mateka. Baada ya Wafaransa kushindwa vibaya kwa mara ya kwanza barani Afrika, nchi hiyo ililazimika kusalimu amri na kuomba yafanyike makubaliano ya amani. Hata hivyo Amir Abdulqadir Jazairi alikataa ombi hilo hadi baada ya miaka miwili iliyofuata, ambapo alifanikiwa kukomboa karibu ardhi yote ya Algeria kutoka katika mikono ya Wafaransa.
Na miaka 798 iliyopita katika siku sawa na ya leo Abubakar Muhyiddin Muhammad mashuhuri kwa jina la Ibn Arabi, arif na msomi mkubwa wa Kiislamu aliaga dunia huko Damascus. Alizaliwa mwaka 560 Hijria huko Andalusia, Uhispania ya leo. Ibn Arabi alifanya safari nyingi katika baadhi ya nchi na miji ikiwemo Tunisia, Makka na Baghdad na kila alipofika aliheshimiwa na kukirimiwa. Alikuwa msomi hodari na baadhi ya duru zinasema kuwa ameandika vitabu na risala zaidi ya 500. Miongoni mwa kazi zake kubwa ni vitabu vya "Tafsir Kabir", "al Futuhatul Makkiyyah" na "Fususul Hikam".
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)