TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Ikulu ya rais Somalia yashambuliwa na Ash-Shabab

Ikulu ya rais Somalia yashambuliwa na Ash-Shabab Kundi la kigaidi la ash-Shabab nchini Somalia, limetekeleza shambulizi dhidi ya ikulu ya rais wa nchi hiyo na kupelekea mtu mmoja kuuawa. Mbali na kuthibitisha habari hiyo, afisa usalama wa nchi hiyo Abdur Rahman Muhammad amesema kuwa makombora manne yaliipata ikulu hiyo ya rais huyo wa Somalia mapema leo. Kundi la ash-Shabab limetangaza kuhusika na shambulizi hilo. Taarifa iliyotolewa na kundi hilo imesema kama ninavyonukuu: “Tumeshambulia ikulu, na baadhi ya makombora yamefanikiwa kuipata ikulu hiyo.” Mwisho wa kunukuu. Polisi imethibitisha tukio hilo na kuahidi kuwachukulia hatua kali wahusika. Hivi karibuni kundi la ash Shabab la Somalia lilisambaza mkanda wa video likitishia kufanya mashambulizi mengine ya kigaidi katika nchi kadhaa ikiwemo Kenya. Weledi wa mambo wanasema hatua hiyo kuwa imetokana na hasira za kundi hilo kufuatia kupoteza maeneo mengi liliyokuwa likiyadhibiti yakiwemo yale ya kistratijia nchini Somalia. Kwa hivyo shambulizi la mjini Mogadishu dhidi ya ikulu ya Rais Hassan Sheikh Mohamed, linatoa ujumbe kwamba kundi hilo bado lingali na uwezo nchini Somalia.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)