TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Ubelgiji: Tutaisaidia Kongo DRC katika uchaguzi

Ubelgiji: Tutaisaidia Kongo DRC katika uchaguzi Serikali ya Ubelgiji imetangaza kuwa itaisaidia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa ajili ya kuandaa ratiba ya uchaguzi ujao nchini humo. Didier Reynders, Waziri Mkuu wa Ubelgiji na ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo amesema kuwa, nchi yake ipo tayari kuisaidia Kinshasa kwa ajili ya kuandaa ratiba ya wakati wa kufanyika wa uchaguzi huo. Akizungumza na vyombo vya habari mjini Kinshasa alipokuwa katika siku ya mwisho ya safari yake nchini humo, Didier alisema kuwa suala la usalama wa maeneo ya mashariki mwa Kongo linahitajia kuwekewa ratiba madhubuti itakayosaidia kuhakikisha uchaguzi ujao unafanyika katika mazingira salama. Tarehe 12 mwezi huu, tume ya taifa ya uchaguzi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ilisambaza ratiba ya uchaguzi, ratiba ambayo hata hivyo ilikosolewa na viongozi wa vyama vya upinzani nchini humo. Kwa mujibu wa viongozi wa vyama hivyo vya upinzani, haitowezekana kupatikana kiwango cha dola bilioni moja za kugharamia uchaguzi mkuu kama ilivyopangwa. Didier Reynders, Waziri Mkuu wa Ubelgiji amesema utengaji wa bajeti inayohitajika kwa ajili ya uchaguzi huo unapasa uanze haraka iwezekanavyo. Akiashiria mauaji ya watu 260 katika mapigano yaliyojiri mjini Beni mashariki mwa Kongo, kati ya mwezi Oktoba na Disemba mwaka jana, Reynders amesema kuwa, ni suala la dharura kuhakikisha uchaguzi unafanyika katika mazingira salama. Weledi wa mambo wameitaja safari ya ujumbe huo wa Ubelgiji nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuwa ni uingiliaji wa mambo ya ndani ya taifa hilo.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)