TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Jeshi la Kongo DRC lashambulia ngome za waasi

Jeshi la Kongo DRC lashambulia ngome za waasi Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limeendeleza operesheni zake dhidi ya waasi wa Rwanda wa FDLR kwa kushambulia ngome za waasi hao mashariki mwa nchi hiyo kubwa ya katikati mwa Afrika. Afisa mmoja wa jeshi ambaye anashiriki kwenye operesheni hizo katika hifadhi ya taifa ya Virunga, amesema kuwa, baada ya kutolewa amri ya kuwashambulia waasi hao wa Kihutu, askari wa serikali walianzisha mashambulizi makali na kufanikiwa kukomboa maeneo mengi kutoka kwa waasi hao. Mashirika kadhaa yasiyo ya kiserikali mjini Kivu yamethibitisha habari hiyo. Kwa mujibu wa habari, operesheni hizo zinafanyika katika eneo la Mabenga, Rutshuru kwenye mpaka wa Kongo na nchi za Rwanda na Uganda. Mapigano makali ya jana yalitokea katika milima ya maeneo hayo ambapo jeshi lilifanikiwa kukomboa vijiji viwili kutoka mikononi mwa waasi hao wa Rwanda.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)