TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

LEO KATIKA HISTORIA 15 Februari,

Jumapili, 15 Februari, 2015 
 Leo ni Jumapili tarehe 25 Mfunguo Saba Rabiu th-Thani mwaka 1436 Hijria, sawa na tarehe 15 Februari mwaka 2015 Miladia.
Siku kama ya leo, miaka 1148 iliyopita, alifariki dunia Al-Ṣabi Thābit ibn Qurra, mtaalamu wa hesabati, mnajimu na tabibu wa kipindi cha utawala wa Abbasiya. Ibn Qurra alizaliwa mwaka 221 Hijiria, mjini Harran, Iraq, na kujifunza lugha za Kigiriki, Syriac na Kiarabu. Baadaye msomi huyo alielekea mjini Baghdad kwa ajili ya kujiendeleza zaidi kimasomo ambapo alitokea kuwa mtaalamu mkubwa wa hesabati na mnajimu mashuhuri wa Kiislamu.
*******
Siku kama ya leo miaka 26 iliyopita, Jeshi Jekundu la Shirikisho la Urusi ya Zamani lililazimika kuondoka nchini Afghanistan baada ya kuikalia kwa mabavu nchi hiyo kwa miaka kumi. Majeshi hayo yaliondoka baada ya kushindwa kukabiliana na muqawama wa mujahidina wa Kiislamu. Lengo la Umoja wa Sovieti la kuivamia na kuikalia kwa mabavu Afghanistan mwaka 1979, lilikuwa ni kuizatiti na kuitia nguvu serikali kibaraka ya Kabul iliyokuwa ikiungwa mkono na Moscow na kueneza satua yake upande wa maeneo ya kusini mwa Asia. Hatua hiyo iliyoyatumbukiza hatarini maslahi ya Marekani, ilikabiliwa na radiamali kali ya Washington ambapo Ikulu ya Marekani (White House) ilianzisha operesheni za kuyatoa majeshi ya Umoja wa Sovieti huko Afghanistan. Hatimaye baada ya miaka 10 wananchi wa Afghanistan wakisaidiwa na Mujahidina walifanikiwa kuhitimisha uvamizi huo na kuyatoa majeshi ya Urusi katika ardhi yao.
*******
Miaka 233 iliyopita kwa mujibu wa kalenda ya Miladia, vilianza vita vya majini kati ya Ufaransa na Uingereza katika pwani ya India. Vita hivyo vilivyodumu kwa muda wa miezi saba, vilikuwa ni mlolongo wa vita kati ya nchi mbili hizo vilivyokuwa na lengo la kuikoloni India na kupora utajiri wake. Ijapokuwa Ufaransa ilishinda vita hivyo, lakini nchi hiyo haikuweza kurejea India na kuikoloni nchi hiyo, na badala yake Uingereza ilibaki na kuendelea kuwa mkoloni mkuu huko Bara Hindi.
*******
Na siku kama ya leo miaka 207 iliyopita, mfalme wa Urusi ya zamani aliidhibiti kikamilifu nchi ya Finland. Katika karne 11 Miladia, Finland ambayo ilikuwa inakaribiana na dola kubwa la Urusi ya Zamani na ilikuwa inahisi hatari kutoka kwa jirani huyo, iliomba msaada kutoka kwa Sweden ambayo ilikuwa ikishindana na Urusi. Suala hilo lilipelekea Sweden nayo kuidhibiti Finland katika karne ya 15 Miladia na baada ya kudhoofika Sweden na satwa kuchukuliwa ya Urusi, sehemu kadhaa za Finland ziliangukia mikononi mwa Warusi na hatimaye nchi hiyo ikadhibitiwa kikamilifu na Urusi ya Zamani kwenye siku kama ya leo na baada ya kupita karibu miaka 650 ya kudhibitiwa na Sweden.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)