TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Michuano ya Vilabu Afrika yapamba moto

Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Kombe la Klabu Bingwa na Kombe la Shirikisho, timu za Azam na Yanga zimeanza vema safari yao ya kuwania makombe hayo baada ya kila timu kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wapinzani wao.

Ushindi huo unairahisishia Yanga kusonga mbele katika mchezo wa marudiano utakaofanyika mjini Gaborone wiki mbili zijazo.

Wachezaji wa timu ya Azam ya Tanzania wakifurahia ushindi dhidi ya El-Merrekh ya Sudan kwa kuifunga 2-0 katika mchezo uliofanyika Jumapili nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam
Nao Azam, wawakilishi katika kombe la klabu bingwa imeanza kampeni yake kwa kuinyuka El Merreikh ya Sudan kwa magoli 2-0 katika mchezo uliofanyika uwanja wa Azam Complex Chamazi, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Mabao ya Azam yalifungwa na Didier Kavumbagu na John Bocco.
Azam wa
 natarajiwa kurudiana na El-Merreikh mjini Khartoum, wiki mbili zijazo.
Gor Mahia ya Kenya iliyoizamisha CNaps Sport ya Madagascar bao 1-0 katika mchezo wao wa awali uliochezwa Jumamosi mjini Nairobi
Matokeo ya timu nyingine za ukanda wa Afrika Mashariki katika Kombe la Shirikisho la CAF, Polisi Zanzibar imekumbana na kipigo kizito baada ya kuangushiwa mzigo wa mabao 5-0 dhidi ya CF Mounana ya Gabon na hivyo kujiweka katika mazingira magumu ya kuendelea hatua ya pili.
Sofapaka ya Kenya nayo imepoteza mchezo wake wa kwanza dhidi ya Platinum ya Zimbabwe kwa kuchapwa magoli 2-1. Rayon Sport ya Rwanda imepata ushindi ugenini kwa kuifunga Panthere ya Cameroon goli 1-0. Nayo URA ya Uganda imepata ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Elgeco Plus ya Madagascar.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)