TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Italia yawaokoa maelfu ya wahamiaji




 Kikosi cha ulinzi wa pwani ya Italia kimesema kimewaokoa zaidi ya wahamiaji elfu mbili wakisafiri katika maboti katika bahari ya Mediterani-- katika operesheni kubwa kuliko zote kufanywa kwa wakati mmoja mpaka sasa.
Meli za jeshi la wanamaji wa Italia na meli za mizigo za kibiashara pia zilizuhiska katika operesheni hiyo.
Kikosi cha walinzi wa pwani kinasema kwa mara ya kwanza walikabiliana na watu wenye silaha wanaofanya biashara ya kusafirisha watu na kuhatarisha maisha ya wafanyakazi wake.
Wengi wa wahamiaji ambao waliondoka kutoka Libya na kujaribu kufika kisiwa cha Lampedusa -- walikuwa vijana kutoka nchi za Afrika. (wiki iliyopita zaidi ya wahamiaji mia tatu wanadhaniwa kufa baharini.).
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)