TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Ndege za kivita za Nigeria zashambulia Boko Haram

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhPl6_2MI9b98DyQEBumPxENBXm111RJeLC9_kngqdTGRgMgNXijdXnhw5RgcnkJJQQ8Uifd2P8eDaYRh6E8WahaSJmkNnEKQKKoWY6EibMBauZagY00GCqzOvZPf2rEhcMUJbm0k3A9ug/s1600/us-military-plane.jpgNdege za kivita za Nigeria jana zilizishambulia kambi za mafunzo, maficho ya silaha na magari ya wanamgambo wa kundi la Boko Haram katika msitu wa kaskazini mashariki wa Samibisa. Msemaji wa jeshi la Nigeria Meja Jenerali Chris Olukolade amesema kuwa wanamgambo wengi wa kundi la Boko Haram wameuliwa kwenye mashambuliz hayo huku wengine wakikimbilia katika maeneo mbalimbali ya msitu na nje ya kambi zao za mafunzo zilizoshambuliwa.  
Baada ya kupita mwaka mmoja ambapo wanamgambo wa Boko Haram wameonekana kusonga mbele huku wakiteka maeneo mengi, kuua maelfu ya watu na kuwateka nyara mamia ya wengine, wengi wakiwa ni wanawake na watoto, hali ya mambo ilionekana kuwageukia mwezi uliopita, baada ya nchi kadhaa jirani na Nigeria kuamua kuanzisha mashambulizi dhidi ya kundi hilo. Vikosi vya Nigeria vimetangaza kuwa vimewauwa wanamgambo wa Boko Haram zaidi ya 300 katika oparesheni iliyofanywa na jeshi hilo ya kuikomboa miji na vijiji 11 tangu mwanzoni mwa wiki hii.  
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)