TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

LEO KATIKA HISTORIA Ijumaa, Februari 20

Ijumaa, Februari 20, 2015 Leo ni Ijumaa tarehe Mosi Jamadil Awwal 1436 Hijria sawa na Februari 20, 2015.
Miaka 27 iliyopita katika siku kama ya leo, inayosadifiana na tarehe Mosi Esfand 1366 Hijria Shamsia, ndege moja ya abiria ya Iran ilishambuliwa na kutunguliwa kwa kombora la majeshi ya utawala wa kidikteta wa Saddam Hussein wa Iraq na kuangushwa, wakati wa vita vya Iran na Iraq. Katika tukio hilo, Hujjatulislam Fadhlullah Mahallati, mwakilishi wa Imam Khomeini kwenye Kikosi cha Kulinda Mapinduzi ya Kiislamu (Sepah) aliuawa shahidi akiwa pamoja na viongozi na wabunge 39 wa Iran.
Siku kama ya leo miaka 68 iliyopita, inayosadifiana na tarehe 20 Februari 1947, Uingereza hatimaye ilikubali kuipatia India uhuru wake baada ya kuikoloni nchi hiyo kwa karne mbili. Uhuru wa India ulipatikana kutokana na mapambano ya muda mrefu yaliyoongozwa na Mahatma Gandhi. Katika kipindi chote cha utawala wake wa kikoloni huko India, Uingereza ilipora utajiri na maliasili ya nchi hiyo na kuwasababishia hasara kubwa raia wa India. Mwezi Agosti mwaka huohuo India na Pakistan zilitengana na kuwa nchi mbili.
Na miaka 225 iliyopita siku kama ya leo yaani mwaka 1211 Hijiria, alifariki dunia mshairi mkubwa wa Kiislamu Sheikh Kadhim Tamimi Baghdadi, maarufu kwa jina la Azri akiwa na umri wa miaka 80. Alikuwa msomi na mwafasihi mkubwa na ameacha diwani ya mashairi. Miongoni mwa mshairi ya malenga huyu maarufu wa Kiislamu ni shairi maarufu la "Al Azriya" ambalo linamsifu Mtukufu Mtume Muhammad (saw) na kizazi chake kitukufu na kubainisha misingi ya dini ya Uislamu. Shairi hilo lina zaidi ya beti 1000.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)