TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Uchaguzi wa bunge Misri huenda ukaakhirishwa

Uchaguzi wa bunge Misri huenda ukaakhirishwa Uchaguzi wa bunge nchini Misri uliopangwa kufanyika mwezi ujao wa Machi huenda ukaahirishwa baada ya kushitadi malalamiko kutoka kwa wanaharakati wa kisiasa na kijamii wanaopinga sheria za sasa za uchaguzi. Wataalamu wa sheria wanasema sheria za uchaguzi zinakinzana na katiba ya nchi kwani kipengee cha 37 cha sheria hizo kinamzuia raia wa Misri aliye na uraia pacha kugombea wadhifa wa ubunge ilihali katiba haijaweka kizuizi hicho. Issam Islambuli, mwanaharakati wa kutetea haki za raia wa nchini Misri amesema kuwa, sheria ya uchaguzi imetenga viti 8 kwa Wamisri wanaoishi nje ya nchi ilihali idadi yao ni takriban milioni 10 na kwa mantiki hiyo viti hivyo haviendani na idadi hiyo na kwamba pana haja ya sheria hiyo kufanyiwa maekebisho.
Wamisri waishio nje ya nchi wanatarajiwa kuanza kupiga kura kuwachagua wabunge wao kuanzia Machi 21 mwaka huu.
Huku hayo yakijiri, habari za hivi punde zinasema kuwa mlipuko mkubwa wa bomu umetokea katika mji mkuu wa Misri, Cairo na hadi sasa Wizara ya Afya inasema mtu mmoja amethibitishwa kufariki dunia.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)