TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

UN: Waislamu wanaendelea kubaguliwa Myanmar

UN: Waislamu wanaendelea kubaguliwa Myanmar Kamisheni Kuu ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imeeleza wasiwasi kuhusu ongezeko la ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Myanmar na kusema kuwa matukio yaliyojiri hivi karibini nchini humo ni kinyume na ahadi ya serikali ya nchi hiyo ya kuheshimu haki za kiraia za makundi yote ya waliowachache hususan Waislamu milioni moja wa Rohingya.
Taarifa iliyotolewa jana na Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Zeid Ra'ad Zeid Al-Hussein imesema kuwa uamuzi uliochukuliwa na Rais wa Myanmar wa kufuta utambulisho wa raia wasio Mabudha ni ukiukaji wa wazi wa haki za kiraia. Zeid Ra'ad Zeid Al-Hussein amesema maafisa wa serikali ya Myanmar wanakataza hata kutumiwa neno la Rohingya ambalo linaarifisha utambulizho wa Waislamu wa nchi hiyo na kwamba jambo hilo linatia wasiwasi. Taarifa hiyo ya afisa wa Umoja wa Mataifa imesema kuwa Waislamu milioni moja wa Manmar wanaishi katika hali ya kusikitisha na kwamba laki moja na 40 elfu miongoni mwao wamelazimika kukimbia makazi yao kutokana na mbinyo mkali wa serikali ya Myanmar.
Katika hatua mpya ya kuwakandamiza Waislamu, Rais wa Myanmar ameamuru kubatilishwa vitambulisho vya Waislamu wote nchini humo na kuwazuia kushiriki katika uchaguzi ujao.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)