TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Ki-moon awataka Salva Kiir na Machar waelewane

Ki-moon awataka Salva Kiir na Machar waelewane Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amemtaka Rais Salva Kirr wa Sudan Kusini na kiongozi wa waasi Riek Machar kufikia makubaliano kwa kwa shabaha ya kuupatia ufumbuzi jumla mgogoro wa nchi hiyo changa zaidi barani Afrika. Ban Ki-moon amesisitiza kwamba, pande mbili hasimu huko Sudan Kusini zinapaswa kufikia makuabaliano na kuhitimisha mgogoro wa nchi hiyo. Amesema hayo ikiwa kesho ndio siku ya mwisho ya muhula uliotolewa na Jumuiya ya Kieneo ya IGAD kwa pande mbili hasimu huko Sudan Kusini ziwe zimefikia makubaliano. Duru ya mwisho ya mazungumzo ya amani kwa upatanishi wa Jumuiya ya Kieneo ya IGAD inatarajiwa kufikiwa kesho. Licha ya juhudi kubwa za IGAD katika upatanishi wa mgogoro wa Sudan Kusini, hadi sasa pande hizo hazijafikia makubaliano ya kuhitimisha mgogoro huo. Wakati huo huo, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeunga mkono azimio la kuziwekea vikwazo pande mbili hasimu za Sudan Kusini, endapo hazitafikia makubaliano katika muda ulioainishwa unaomalizika kesho.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)