TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Kenyatta aanza ziara ya siku tatu nchini Uganda

Kenyatta aanza ziara ya siku tatu nchini UgandaRais Uhuru Kenyatta wa Kenya Jumamosi ya leo ameanza ziara ya siku tatu katika nchi jirani ya Uganda. Katika safari yake hiyo Rais Kenyatta anatarajiwa kukutana na mwenyeji wake Rais Yoweri Museveni ambapo viongozi hao wanatarajiwa kufanya mazungumzo kuhusiana na uhusiano wa pande mbili na masuala ya kibiashara.
Marais hao wanatarajiwa pia kubadilishana mawazo kuhusiana na hali ya Sudan Kusini na vilevile hali ya mambo nchini Burundi ambapo Rais Museveni ni mpatanishi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika mgogoro wa kisiasa nchini humo.
Akiwa nchini Uganda Rais Kenyatta mbali na kukutana na jumuiya ya wafanyabiasha wa Uganda atakutana pia na Wakenya wanaoishi nchini humo. Taarifa zaidi zinasema siku ya Jumatatu Rais wa Kenya anatarajiwa kulihutubia Bunge la Uganda.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)