TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Watoto 2 wafariki katika ajali Ziwa Victoria Kenya

Watoto 2 wafariki katika ajali  Ziwa Victoria KenyaWatu wawili wamethibitishwa kufariki dunia, wengine zaidi ya 20 kuokolewa, na wengine kadhaa hawajulikani walipo baada ya kivuko kilichokuwa na watu 200 kugongana na meli ya uvuvi mapema leo kwenye Ziwa Victoria, magharibi mwa Kenya.
Kamanda wa polisi kaunti ya Homa Bay John Omusanga amesema, watoto wawili wamefariki kwenye ajali hiyo iliyotokea saa nane usiku karibu na kisiwa cha Remba. Watoto hao wametambuliwa kwa majina ya Fatou Bensouda, aliyekuwa na umri wa miaka 2, na Eda Anyango alioyekuwa na umri wa miaka 4. Kamanda wa polisi wa mkoa wa Nyanza Willy Lugusa amesema, wengi wa watu walionusurika waliokolewa na wavuvi. Amesema chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika.
Shirika la msalaba mwekundu nchini Kenya linaongoza operesheni ya uokoaji, na idadi ya vifo huenda ikaongezeka kwa kuwa watu wengi bado hawajulikani walipo.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)