TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Baraza la Usalama lajadili hali ya mambo Libya

Baraza la Usalama lajadili hali ya mambo Libya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, leo limefanya kikao kujadili hali ya mambo nchini Libya. Akizungumza kwa njia ya video kutoka Roma, Italia, Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu na Mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa , Bernadino Leon amesema ni dhahiri kuwa ugaidi unatishia hali ya usalama nchini Libya, kufuatia mashambulizi yaliyofanywa na kundi la kigaidi  la Daesh (ISIL) dhidi ya watu wa matabaka mbali mbali.
Ameongeza kuwa taifa la Libya halina uwezo thabiti wa kukabiliana na changamoto inayotolewa na ugaidi, akitaja haja ya kuzingatia ombi la nchi jirani za Libya la kupatiwa msaada wa kimataifa. Leonamesema ni muhimu kwa jamii ya kimataifa kusaidia juhudi za Libya za kukabiliana na ugaidi.Mwakilishi huyo wa Umoja wa Mataifa amesema timu za mazungumzo zitaanza kukutana leo nchini Morocco, ili kuridhia ajenda ya awamu ijayo ya mazungumzo yenye lengo ya kurejesha amani na utulivu nchini Libya. Katika kikao hicho, Balozi wa Libya katika Umoja wa Mataifa Ibrahim Dabbashi ametoa wito kwa Baraza la Usalama kuondoa vikwazo dhidi ya nchi yake ili iweze kununua silaha za kukabiliana na magaidi wa kitakfiri wa Daesh.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)