TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Evans na Cisse kuadhibiwa kwa kutemeana Kohozi

Mlinzi wa Manchester United Jonny Evans na Mshambulizi wa Newcastle United Papiss Cisse huwenda wakaadhibiwa vikali baada ya kutemeana makohozi katika mechi ngumu baina yao jana usiku.
Kulingana na wandani wa maswala ya nidhamu katika ligi hiyo ya Uingereza,wawili hao huwenda wakapigwa marufuku ya mechi sita kila mmoja.
Refarii Anthony Taylor aliwaonya wawili hao lakini hakuchukua adhabu yeyote dhidi yao.
Sasas shirikisho la Kandanda la Uingereza linasubiri ripoti ya refarii huyo ilikubaini hatua ipi itawafaa vibonde hao wawili.
Msimu uliopita George Boyd alipigwa marufuku ya mechi 3 kwa kumtemea kohozi kipa ya Manchester City Joe Hart.
 
 Msimu huu hata hivyo sheria mpya zinasema kuwa adhabu iwe maradufu ya hiyo ili iwe ni funzo dhidi ya yeyote atakayekuwa mtundu uwanjani.
Cisse ambaye mwezi Desemba alipigwa marufuku kwa kumshambulia kiungo wa Everton Seamus Coleman.
Kwa mujibu wa wachezaji wakongwe Evans na Cisse wanastahili adhabu kali.
Meneja wa Newcastle John Carver na Louis van Gaalwa Manchester United hawakusema lolote kuhusiana na tukio hilo.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)