TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Al-Sisi amfuta kazi Waziri wa Mambo ya Ndani Misri

Al-Sisi amfuta kazi Waziri wa Mambo ya Ndani Misri Rais Abdul Fattah al Sisi wa Misri amemfukuza kazi Waziri wa Mambo ya Ndani Mohamed Ibrahim na badala yake amemteua Magdi Abdul Ghaffar kujaza nafasi hiyo. Meja Jenerali Magdi Abdul Ghaffar alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa ya Misri. Kufutwa kazi Waziri wa Mambo ya Ndani wa Misri ni katika sehemu ya mabadiliko ya baraza la mawaziri la nchi hiyo yaliyozijumuisha wizara nane, miongoni mwao ni pamoja na wizara za elimu, afya, kilimo, utalii na utamaduni. Waziri huyo aliyefutwa kazi ambaye awali aliteuliwa wakati kulipofanyika marekebisho katika baraza la mawaziri la Misri mwezi Januari mwaka juzi, amekuwa akikosolewa vikali kwa nafasi yake kuu katika kuwakandamiza wapinzani.  Waziri wa Mambo ya Ndani wa Misri aliyefutwa kazi na Rais al Sisi alikuwa mmoja wa mawaziri wachache walioweza kuhifadhi nyadhifa zao baada ya Mohamed Morsi, Rais halali wa nchi hiyo kupinduliwa na jeshi mwezi Julai mwaka juzi.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)