TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Mafuriko Dar: Watu watano wapoteza maisha

Mafuriko Dar: Watu watano wapoteza maishaNchini Tanzania watu watano wamefariki dunia na maelfu ya wengine wamepoteza makazi yao, huku usafiri katika mji mkuu Dar es salaam ukikwama kutokana na mvua kubwa zilizonyesha kuanzia Jumanne.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Bw Meck Sadik amesema kati ya waliofariki ni watoto wawili na mzee mmoja, ambao walisombwa na mafuriko.
Amesema kwa sasa serikali inafanya tathmini kuhusu hasara iliyosababishwa na mafuriko hayo, lakini ripoti ya awali inaonesha kuwa zaidi ya nyumba 38 katika eneo la Kigamboni ziliathiriwa vibaya na mafuriko.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa ya Tanzania Bibi Agnes Kijazi amesema mvua hizo ni za msimu. Ameongeza kuwa mifumo ya hali ya hewa inaonyesha kuwa “hali ya mvua inatarajiwa kuendelea katika baadhi ya siku hadi Mei 20, mwaka huu”. Mikoa ya Tanga, Pwani, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba pia vinatarajiwa kuwa na mvua kali.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)