TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMATANO 19.08.2015

Chelsea watajaribu kuwazidi kete Manchester United katika kumsajili mshambuliaji wa Barcelona Pedro, 28 (Mail), Chelsea watafikiria kuongeza dau na kufikia pauni milioni 40 kumsajili beki wa Everton John Stones, 21, baada ya dau la pauni milioni 30 kukataliwa (Guardian),Fernabahce watamshawishi beki wa Chelsea John Terry na mshahara wa pauni milioni 2.5 kwa mwaka ili ahamia Uturuki (Mail), Branislav Ivanovic, 31, huenda akawekwa bench na Jose Mourinho baada ya Chelsea kumsajili Abdul Baba Rahman ambaye anaweza kuanza siku ya jumapili dhidi ya West Brom (Mirror), Manchester City watakamilisha usajili wa pauni milioni 88 kwa beki wa Valencia Nicolas Otamendi na Kevin De Bryce (Mirror), West Brom wamewaambia Tottenham kuwa watahitaji kutoa pauni milioni 25 kumsajili Saido Berahino, 22 (Independent), Bournemouth wanataka kumsajili mshambuliaji wa Sunderland Jermain Defoe, 32, ambaye aliwahi kuichezea klabu hiyo akiwa bado kijana (Mirror), Arsenal watahitaji kulipa pauni milioni 35 kama wanataka kumsajili mshambuliaji wa PSG Edinson Cavani (Eurosport), Real Madrid wana matumaini kuwa wanaweza kumtumia kipa Keylor Navas, 28, katika jitihada zao za kutaka kumsajili kipa wa Manchester United David De Gea, 24 (Marca), rais wa AC Milan Silvio Berlusconi amemwambia mshambuliaji wa PSG Zlatan Ibrahimovic, 33, kuwa anasubiriwa kwa "moyo mkunjufu" kurejea San Siro (Gazzetta World). NA

 Manchester United wanajaribu kumsajili winga wa Southampton Sadio Mane. Dau la kumtaka mchezaji huyo wa kimataifa wa Senegal, 23 liliwasilishwa wiki iliyopita. Mshambuliaji wa Barcelona, Perdo, alikuwa akinyatiwa na United, lakini sasa anakaribia kujiunga na Chelsea kwa pauni milioni 21. Mane alipachika mabao 10 katika mechi 32 msimu uliopita baada ya kujiunga na Southampton akitokea Red Bull Salzburg. Mane pia alipachika "Hat Trick" ya haraka zaidi katika historia ya Ligi Kuu ya England.

 Beki wa kati wa Barcelona, Gerard Pique amefungiwa kucheza mechi nne baada ya kuoneshwa kadi nyekundu kwa kumtukana mwamuzi wa pembeni kwenye mchezo wa Super Cup dhidi ya Athletic Bilbao siku ya Jumatatu. Barcelona wanaweza kukata rufaa, na adhabu hiyo kupunguzwa, lakini ikikataliwa, mchezaji huyo wa kimataifa wa Spain atakosa mechi nne za mwanzo za La Liga. Pique aliomba radhi kwa kupewa kadi nyekundu siku na Jumanne, lakini anakanusha kutumia lugha chafu.


Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)