TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Ugiriki iko tayari kunusuru uchumi wake

Serikali ya Ugiriki imeleezea imani yake kwamba mkataba kuhusu madeni yake, utafikiwa ndani ya saa arobaini na nane, licha ya kupinga muda wa mwisho uliowekwa na nchi za Ulaya zinazotumia sarafu ya euro.

http://www.dw.de/image/0,,18227293_404,00.jpg
 Mkutano wa mawaziri kutoka nchi za Ulaya zinazotumia sarafu ya euro waliokutana mjini Brussels, Ubalegiji ulivunjika mapema kuliko ulivyotarajiwa wakati serikali ya Ugiriki kutupilia mbali fursa iliyotolewa kwa nchi hiyo hadi Ijumaa kuhusu mpango wa nchi hiyo kudhaminiwa, au kuona mipango ikiisha kufikia mwishoni mwa mwezi huu.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya serikali ya Ugiriki vinasema pendekezo la nchi za ulaya ni "upuuzi" na "halikubaliki".
Lakini waziri wa fedha wa Ugiriki, Yanis Varoufakis, amesema Ulaya itafanya "ulaghai uliozoeleka" kwa kutumia mkataba usio na ufumbuzi wa hali iliyopo.
Serikali ya Ugiriki inataka kumaliza masharti iliyowekewa katika deni lake la euro bilioni mia mbili na arobaini. Lakini bila ya fedha za nyongeza kufikia mwishoni mwa mwezi, inaweza kukosa fedha.)
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

1 comments:

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)