TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Rasimu ya azimio la kupambana na Boko Haram katika Baraza la Usalama

Rasimu ya azimio la kupambana na Boko Haram katika Baraza la Usalama Nchi tatu za Kiafrika zimewasilisha katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa rasimu ya azimio la kuunga mkono mapambano ya kieneo dhidi ya kundi la kigaidi la Boko Hram la nchini Nigeria. Rasimu hiyo iliyowasilishwa na Nigeria, Chad na Angola inasisitiza juu ya uungaji mkono wa kifedha na suhula za dharura kwa askari wa kimataifa kwa lengo la kupambana na kundi hilo la kitakfiri na kigaidi la Boko Haram. Mwezi Januari mwaka huu Umoja wa Afrika ulikaribisha pendekezo la nchi jirani na Nigeria la kuunda kikosi cha kieneo kwa ajili ya kupambana na Boko Hram na limeafiki suala la kuongezwa askari wa kikosi hicho kutoka askari 8700 hadi 10,000.
Hivi sasa wanachama 15 wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wameunga mkono kikosi hicho kitakachobuniwa na nchi za Nigeria, Cameroon, Chad, Niger na Benin. Iwapo rasimu iliyowasilishwa na nchi tatu zilizotajwa itapasishwa na kuwa azimio katika Baraza la Usalama, basi baraza hilo litaadhibu watu au nchi yoyote itakayounga mkono Boko Haram. Lengo la kubuniwa kikosi hicho ambacho kitatekeleza majukumu yake kwa mwaka mmoja litakuwa ni kurejesha amani katika mipaka ya nchi jirani na Nigeria ambazo ni Chad, Cameroon, Niger na Benin. Kuenea kwa vitendo vya uagaidi vya wanamgambo wa Boko Haram katika maeneo ya kaskazini mashariki mwa Nigeria na kuvuka mpaka hadi kwenye ardhi za nchi jirani kama vile Niger na Chad kumewapelekea viongozi wa nchi hizo wafikirie juu ya njia za kubuni kikosi cha kieneo cha kukabiliana na magaidi hao wanaosababisha mauaji na hasara kubwa katika eneo. Tokea mwezi Februari uliopita jeshi la Nigeria limekuwa likishirikiana na askari wa Chad, Cameroon na Niger katika kupambana na wanamgambo wa Boko Haram. Wakati huohuo siku ya Alkhamisi vyombo vya kijeshi vya Nigeria vilitoa habari za kusafishwa baadhi ya miji ya majimbo matatu ya kaskazini mashariki mwa Nigeria kutokana na magaidi hao wa kitakfiri. Badhi ya miji hiyo ni mji wenye wakazi wengi wa Kikristo wa Madagali ambao ulitekwa na kudhibitiwa na Boko Haram mwezi Agosti mwaka uliopita. Akizungumza hivi karibuni na waandishi, Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria ametabiri kuwa majimbo mawili ya Adamawa na Yobe yatakombolewa katika kipindi cha majuma mawili yajayo na jumbo la Borno katika juma la tatu. Majimbo hayo yalikuwa chini ya sheria kali ya kutotoka nje usiku sheria iliyotangazwa tokea mwezi Mei mwaka 2013. Rais Jonathan alitaka kurefusha kwa mara ya tatu muda wa hali hiyo ya hatari katika majimbo hayo matatu mwezi Novemba uliopita lakini hatua hiyo ikapingwa vikali na wabunge. Hivi sasa operesheni za pamoja zinaendeshwa na askari wa Nigeria, Cameroon, Chad na Niger kwa lengo la kurudisha amani na usalama katika maeneo ya kaskazini mashariki mwa Nigeria kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika nchini humo tarehe 28 mwezi huu. Kutangaza kundi la Boko Haram kuwa linafungamana na kundi jingine la kigaidi la Daesh kumeongeza wasiwasi nchini Nigeria wa kundi hilo kufanya mashambulio makubwa ya kigaidi katika  maeneo tofauti ya nchi hiyo na katika maeneo ya mpaka wa nchi hiyo na nchi jirani katika siku zijazo. Kwa msingi huo viongozi wa nchi jirani ambazo zimeunda muungano wa kieneo dhidi ya Boko Haram wana hamu kubwa ya kuona kuwa rasimu iliyowasilishwa na nchi tatu za Nigeria, Chad na Angola inapitishwa haraka iwezekanavyo katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)