TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Boko Haram washindwa kaskazini mwa Nigeria

Boko Haram washindwa kaskazini mwa Nigeria Jeshi la Nigeria limetangaza kuwa, sehemu kubwa ya maeneo ya kaskazini mashariki mwa nchi hiyo, yamekombolewa kutoka mikononi mwa wanamgambo wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram. Jeshi la nchi hiyo limetangaza kuwa, operesheni pana zilizotekelezwa katika maeneo ya mpakani ya Madagali karibu na jimbo la Borno, kaskazini mwa Nigeria sasa yamekombolewa kutoka kwa wanamgambo hao. Akizungumza Jumatano iliyopita, Rais Good Luck Jonathan wa nchi hiyo alisema kuwa majimbo mawili ya Adamawa na Yobe nayo yatakombolewa wiki chache zilizosalia kutoka kwa wanamgambo wa Boko Haram. Alitabiri kuwa, hadi wiki tatu zijazo jimbo la  Borno pia litakuwa limesafishwa kabisa kutokana na uepo wa wanachama wa kundi hilo linalofahamika kwa kutenda jinai dhidi ya binaadamu nchini humo na nchi jirani. Weledi wa mambo wanazitaja operesheni za majeshi ya muungano wa nchi jirani kwa kushirikiana na jeshi la Nigeria kuwa ni njama za kumsafishia njia kuelekea ushindi katika uchaguzi mkuu ujao nchini Nigeria, Rais Jonathan hasa kwa kuzingatia kuwa, kumekuwepo na tetesi kwamba kiongozi huyo ana ushirikiano na kiongozi mkuu wa kundi hilo la kitakfiri na lenye uelewa potofu wa dini ya Kiislamu, Abubakar Shekau.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)