 
     
    Jeshi la Nigeria limetangaza kuwa, sehemu kubwa ya maeneo ya 
kaskazini mashariki mwa nchi hiyo, yamekombolewa kutoka mikononi mwa 
wanamgambo wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram. Jeshi la nchi
 hiyo limetangaza kuwa, operesheni pana zilizotekelezwa katika maeneo ya
 mpakani ya Madagali karibu na jimbo la Borno, kaskazini mwa Nigeria 
sasa yamekombolewa kutoka kwa wanamgambo hao. Akizungumza Jumatano 
iliyopita, Rais Good Luck Jonathan wa nchi hiyo alisema kuwa majimbo 
mawili ya Adamawa na Yobe nayo yatakombolewa wiki chache zilizosalia 
kutoka kwa wanamgambo wa Boko Haram. Alitabiri kuwa, hadi wiki tatu 
zijazo jimbo la  Borno pia litakuwa limesafishwa kabisa kutokana na uepo
 wa wanachama wa kundi hilo linalofahamika kwa kutenda jinai dhidi ya 
binaadamu nchini humo na nchi jirani. Weledi wa mambo wanazitaja 
operesheni za majeshi ya muungano wa nchi jirani kwa kushirikiana na 
jeshi la Nigeria kuwa ni njama za kumsafishia njia kuelekea ushindi 
katika uchaguzi mkuu ujao nchini Nigeria, Rais Jonathan hasa kwa 
kuzingatia kuwa, kumekuwepo na tetesi kwamba kiongozi huyo ana 
ushirikiano na kiongozi mkuu wa kundi hilo la kitakfiri na lenye uelewa 
potofu wa dini ya Kiislamu, Abubakar Shekau.
   
 
0 comments:
Post a Comment