TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Umoja wa Ulaya wakosoa vikali ubomoaji nyumba za Wapalestina

Umoja wa Ulaya wakosoa vikali ubomoaji nyumba za WapalestinaKushadidi kwa jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel kumekabiliwa na radiamali mbalimbali za kimataifa. Umoja wa Ulaya (EU) umelaani hatua ya utawala haramu wa Israel ya kubomoa nyumba za Wapalestina katika maeneo ya Quds inayokaliwa kwa mabavu. Taarifa ya umoja huo imelaani kubomolewa nyumba za Wapalestina huko Baitul Muqaddas Mashariki na kuitaka Israel ikomeshe vitendo vyake hivyo. Nyumba hizo zipatazo 200 zilikuwa zimejengwa kwa msaada wa fedha uliotolewa na Umoja wa Ulaya. Hivi karibuni, Utawala wa Kizayuni umeshadidisha mashinikizo dhidi ya Wapalestina wanaoishi kwenye maeneo yaliyoanza kukaliwa kwa mabavu na utawala huo ghasibu mwaka 1948. Uporaji wa ardhi, kuwatoa watu majumbani mwao, kubomoa nyumba zao na kupitisha sheria mpya za kibaguzi dhidi ya Wapalestina ni sehemu tu ya hatua zisizo za ubinadamu zinazowanyima Wapalestina hao haki za kijamii na kiuchumi. Radiamali nyengine dhidi ya jinai za utawala wa Kizayuni imetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Nchi za Kiislamu (ISESCO). Abdulaziz bin Othman At-Tawijri amesema Israel ni nembo ya ugaidi na kuongeza kwamba vitendo vya utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina vikiwemo vya uvamizi na ukaliaji wa mabavu, ubomoaji, mauaji, ukandamizaji n.k. vina sura na utambulisho kamili wa kigaidi, na vinakinzana na sheria na hati za kimataifa. Mkurugenzi Mkuu wa ISESCO amesisitiza kwamba kukabiliana na vitendo hivyo vya kinyama vya utawala haramu wa Israel si jukumu la nchi moja maalumu au majimui ya nchi fulani tu bali ni wajibu wa Jamii ya Kimataifa; na uzembe au ajizi yoyote inayofanywa juu ya kukabiliana na ugaidi huo wa kiserikali ina matokeo mabaya yanayotishia amani na usalama wa dunia. Wakati huohuo Kundi la Kiarabu la Ustawi wa Kitaifa lenye makao yake mjini Geneva limekosoa vikali kitendo cha utawala wa Kizayuni cha kutokabidhi viwiliwili vya mamia ya Wapalestina kwa familia zao. Taarifa iliyotolewa siku ya Jumatano na kundi hilo imeeleza kuwa viwiliwili vya watu hao vimezikwa kwa siri kwenye maeneo ya kijeshi ya ardhi za Palestina zilizoanza kukaliwa kwa mabavu mwaka 1948, na hakuna mwenye haki ya kuyakaribia makaburi yao. Kundi la Kiarabu la Ustawi wa Kitaifa limebainisha kwamba katika ulimwengu mzima ni utawala wa Kizayuni pekee ndio ulioweza kufanya vitendo viovu kama hivyo katika kuamiliana na Wapalestina na Waarabu, kwani hata baada ya Wapalestina hao kuuawa shahidi  utawala huo khabithi unaziadhibu familia zao kwa kuwanyima haki ya kuwazika watu wao mahali wanapotaka kwa mujibu wa sheria za dini. Kundi hilo limesisitiza kwamba kitendo hicho cha utawala wa Kizayuni ni jinai ya kidini, kisheria na kimaadili na ni ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa zinazohusiana na haki za binadamu pamoja na Mkataba wa Nne wa Geneva. Kundi la Kiarabu la Ustawi wa Kitaifa limetoa wito kwa jumuiya za kimataifa ziushinikize utawala wa Kizayuni uvikabidhi viwiliwili vya mashahidi hao wa Kipalestina kwa familia zao. Hii ni katika hali ambayo Makarim Wibisono, ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa wa hali ya haki za binadamu katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu ameeleza katika ripoti yake ya hivi karibuni kuhusiana na jinai zilizofanywa na utawala wa Kizayuni mwaka uliopita wa 2014 za mauaji ya zaidi ya Wapalestina 2,000 wakati wa vita vya siku 50 dhidi ya Ukanda wa Gaza, kwamba theluthi moja kati ya waliouawa walikuwa ni watoto wadogo…/
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)