TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Hotuba ya Kiongozi Muadhamu katika kikao na wajumbe wa Baraza la Wataalamu

Hotuba ya Kiongozi Muadhamu katika kikao na wajumbe wa Baraza la WataalamuMkuu wa Wajumbe wa Baraza la Wataalamu wanaomchagua Kiongozi Muadhamu nchini jana walikutana na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullahil Udhma Sayyid Ali Khamenei.
Katika kikao hicho, Kiongozi Muadhamu aliashiria masuala ya sasa katika eneo na changamoto zilizojitokeza kutokana na sera za undumakuwili za nchi za Magharibi. Katika sehemu ya hotuba yake, sambamba na kubainisha sera za kistratijia za Iran katika mazungumzo ya nyuklia, aliashiria pia barua ya hivi karibuni ya maseneta wa Marekani na kusema hiyo ni ishara ya kusambaratika maadili ya kisiasa katika mfumo wa Marekani.
Kiongozi Muadhamu aliongeza kuwa kila wakati unapokaribia muda ulioainishwa kumalizika mazungumzo ya nyuklia, matamshi ya upande wa pili hasa Marekani huwa makali na ya kijeuri zaidi na hii ni sehemu ya ujanja na hila zao. Amesema mbinu hii ni ya kujaribu kukwepa uhalisia wa mambo na kwamba haina faida yoyote ila kufichua njama za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel ambao ndio mmiliki pekee wa silaha hatari za nyuklia katika Mashariki ya Kati.
Jitihada za hivi karibuni za Wazayuni, na hasa Waziri Mkuu wa Utawala wa Kizayuni ambaye alitoa hotuba isiyo na maana katika Bunge la Kongresi Marekani, ni sehemu ya silisila ya njama za Marekani za kutafuta vizingizio ili kukwepa kutekeleza majukumu yake kimataifa. Kama alivosema Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, hatua ya Netanyahu ambaye ni kikaragosi  cha Uzayuni kufika katika Kongresi na kutoa hotuba duni na baada ya hapo  baadhi ya wajumbe wa Kongress kuandika barua inayohusiana na hotuba hiyo, ni siasa zisizo na maana.
Watawala hao wa Marekani na Israel ambao ndio waungaji mkono asili wa magaidi kwa mara kadhaa wameituhumu Iran kuwa inahusika na ugaidi lakini uzoefu umeonyesha kuwa matamshi kama hayo na barua kama hizo haziwezi kubadilisha ukweli wa mambo.
Kama ambavyo Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Mohammad Javad Zarif alivosema, katika kujibu barua ya Maseneta wa Marekani, 'hao maseneta wanapaswa kufahamu kuwa, dunia si Marekani, na kanuni za mahusiano baina ya nchi zinafuata sheria za kimataifa si sheria za ndani za Marekani.'
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika kikao na wajumbe wa Baraza la Wanazuoni Wataalamu alisisitiza kuhusu nukta mbili muhimu. Awali ni kuwa Iran inatekekeza sera za uwazi na ukweli katika mazungumzo ya nyuklia na pia timu ya wanadiplomasia wa Iran katika mazungumzo hayo wanafuata sera hizo. Pamoja na hayo kuna shaka kuhusu mwenendo wa upande wa pili katika mazungumzo. Kama alivyosema Kiongozi Muadhamu, upande wa pili katika mazungumzo ya nyuklia ni hodari kwa kufanya hila, ujanja na usaliti.
Nukta ya pili ni kubainisha utumbulisho uliojaa hadaa wa utawala wa Kizayuni na himaya ya wazi na daima ya mrengo wa wenye misimamo mikali Marekani kwa utawala huu utendao jinai. Lakini hivi sasa utumizi wa mbinu hizo umefika ukingoni. Pamoja na hayo, watu wanaofungamana na mrengo wa Uzayuni katika Kongresi ya Marekani wanajaribu kuibua kelele kwa kisingizio cha kuzuia kile wanachosema kuwa ni 'mkataba mbaya wa nyuklia na Iran. Lengo la Wazayuni na waitifaki wao katika Kongresi ya Marekani ni kupotosha fikra za waliowengi duniani.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)