TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Idadi ya waathirika wa Ebola yapindukia elfu 10

Idadi ya waathirika wa Ebola yapindukia elfu 10 Idadi ya wahanga wa ugonjwa hatari wa Ebola imepindukia elfu 10. Taarifa iliyotolewa na Shirika la Afya Duniani (WHO) jana usiku, imesema kuwa idadi ya watu waliopoteza maisha kwa homa ya ugonjwa huo sasa imefikia watu 10004. Taarifa hiyo imeongeza kuwa, jumla ya watu walioambukizwa maradhi hayo katika nchi za Guinea Conakry, Sierra Leone na Liberia imefikia watu 24,350. Nchi zingine sita zimeripotiwa kupata maambukizi ya ugonjwa huo kwa kusajiliwa visa 15 vya maradhi hayo. Kesi ya kwanza ya maambukizi ya maradhi ya Ebola iliripotiwa mwezi Januari mwaka jana 2014 nchini Guiena Conakry. Wataalamu wa Benki ya Dunia, wametaja hasara inayokaribia dola bilioni moja na milioni 600 za Marekani iliyosababishwa na maradhi hayo. Mwanzoni mwa mwezi huu Shirika la Afya Duniani (WHO) lilitangaza kuanza majaribio ya kwanza ya chanjo ya homa ya Ebola kwa kiwango kipana zaidi nchini Guinea Conakry.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)