 
     
    Idadi ya wahanga wa ugonjwa hatari wa Ebola imepindukia elfu 10. Taarifa
 iliyotolewa na Shirika la Afya Duniani (WHO) jana usiku, imesema kuwa 
idadi ya watu waliopoteza maisha kwa homa ya ugonjwa huo sasa imefikia 
watu 10004. Taarifa hiyo imeongeza kuwa, jumla ya watu walioambukizwa 
maradhi hayo katika nchi za Guinea Conakry, Sierra Leone na Liberia 
imefikia watu 24,350. Nchi zingine sita zimeripotiwa kupata maambukizi 
ya ugonjwa huo kwa kusajiliwa visa 15 vya maradhi hayo. Kesi ya kwanza 
ya maambukizi ya maradhi ya Ebola iliripotiwa mwezi Januari mwaka jana 
2014 nchini Guiena Conakry. Wataalamu wa Benki ya Dunia, wametaja hasara
 inayokaribia dola bilioni moja na milioni 600 za Marekani 
iliyosababishwa na maradhi hayo. Mwanzoni mwa mwezi huu Shirika la Afya 
Duniani (WHO) lilitangaza kuanza majaribio ya kwanza ya chanjo ya homa 
ya Ebola kwa kiwango kipana zaidi nchini Guinea Conakry.
 
                            About 
                            NELSON PASCHAL KAMUGISHA
 
                            This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
                          
 
 
 
0 comments:
Post a Comment